Home Uncategorized NEYMAR KUUNGANA NA MESSI PAMOJA NA SUAREZ BARCELONA: TETESI ZA LEO JUMATANO...

NEYMAR KUUNGANA NA MESSI PAMOJA NA SUAREZ BARCELONA: TETESI ZA LEO JUMATANO HIZI HAPA


Mshambuliaji wa Manchester United Mbelgiji Romelo Lukaku upo tayari kukatwa mshahara ili ahamie klabu ya Inter Milan hivi karibuni. (Gazzetta dello Sport)

Kocha wa Man United Ole Gunnar Solskjaer ameipa klabu yake muda mpaka mwakani kuuza wachezaji wote asiowataka ikiwa kama sehemu ya miango yake ya kuijenga upya klabu hiyo. (MEN)
Barcelona wameamua kuendelea na kocha Ernesto Valverde kwa msimu ujao japo kulikuwa na ripoti kuwa kocha huyo alikuwa afutwe kazi. (Marca)

Rais wa Real Madrid Florentino Perez amesema ana matumaini ya kumsajili Eden Hazard katika majira haya ya joto. (Onda Cero, via Mirror)

Atletico Madrid wamemchagua mshambuliaji wa Paris St-Germain na timu ya taifa ya Uruguay Edinson Cavani kama mbadala wa mshambuliaji wao Diego Costa, 30. (Cadena Ser – in French)
Newcastle United wamefanya mawasiliano na klabu ya Benfica wakiwa na nia ya kumsajili kipa wao ambaye ni raia wa Ugiriki Odysseas Vlachodimos na inaaminika Benfica wanataka kitita cha pauni milioni 13. (O Jogo – in Portuguese)

Barcelona pia inasemekana wapo tayari kumtoa kiungo Philippe Coutinho ama mshambuliaji Ousmane Dembele kwenda Paris St-Germain kama sehemu ya makubaliano ya kumpata mshambuliaji Neymar. (Record)

Kocha wa zamani wa Chelsea Antonio Conte amesaini mkataba mpya wa kuinoa klabu ya Inter Milan mpaka mwaka 2022. (Tuttomercatoweb – in Italian)

Straika wa Eintracht Frankfurt Luka Jovic yaonekana hana nia ya kuendelea kusakata kabumbu kwenye klabu hiyo baada ya kuhamisha viurago vyake kwenye kabati lake la timu kabla ya michuano ya Ulaya ya wachezaji wa chini ya miaka 21. (Bild – subscription)

Kocha wa Arsenal Unai Emery anataka kumsajili beki wa pembeni wa Ubelgiji Thomas Meunier kutoka katika klabu ya Paris St-Germain. (France Football)

SOMA NA HII  ZAHERA ACHANGIA EURO 1000 VIDEO