Home Uncategorized SIMBA FULL SHANGWE LEO WABEBA KOMBE LAO LA 20 TPL

SIMBA FULL SHANGWE LEO WABEBA KOMBE LAO LA 20 TPL


MABINGWA watetezi Simba leo wamekabidhiwa kombe la Ligi Kuu Bara na mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Ndani Kangi Lugola baada ya kumaliza mchezo wao wa mwisho uliochezwa uwanja wa Jamhuri, Morogoro.

Kwenye mchezo wa leo, Mtibwa Sugar wamelazimisha suluhu ya kutofungana wakiwa nyumbani wakiwa na kumbukumbu ya kupoteza kwa kufungwa mabao 3-0 mchezo wa kwanza uliochezwa uwanja wa Uhuru.

Huu ni ubingwa wa 20 kwa Simba wakiwa nyuma ya wapinzani wao wa karibu Yanga ambao wamebeba ubingwa huo mara 27.

Kesho watarejea Dar na kombe hilo huku sherehe zikianzia maeneo ya Kibaha ambapo wachezaji watapanda kwenye gari la wazi wakionyesha kombe walilotwaa  msimu wa mwaka 2018/19 baada ya kufikisha jumla ya pointi 93 wakiwa nafasi ya kwanza.

SOMA NA HII  SIMBA YATAJA SABABU YA KUSHINDWA KUFUNGA MABAO MENGI MBELE YA KAGERA SUGAR

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here