Home Uncategorized KUMEKUCHA AZAM FC, NDAYIRAGIJE KUANZA NA HILI

KUMEKUCHA AZAM FC, NDAYIRAGIJE KUANZA NA HILI


KOCHA wa Azam FC, Etiene Ndayiragije amesema kuwa anahitaji kuboresha kikosi na hesabu zake ni kwenye kuongeza wachezaji wakali wenye uwezo.

Ndayiragije amelamba mkataba wa kuionoa Azam FC akichukua mikoba ya Hans Pluijm kwa kandarasi ya miaka miwili.

“Kutokana na malengo ambayo yapo kwa sasa kazi kubwa itakuwa ni kutengeneza kikosi imara, nina imani hilo linawezekana kutokana na uhitaji ambao upo hivyo kwa kuanza nitaanza na wachezaji kwanza kisha mengine yatafuta.

“Nikifanikiwa kuboresha kikosi itanifanya nifanye kazi kwa wepesi hasa ukizingatia ni timu kubwa na ina kila kitu, hilo linawezekana kikubwa sapoti kwa mashabiki,” amesema. 

SOMA NA HII  AZAM WATINGA KWA MKUU WA MKOA WA LINDI