Home Uncategorized WEMA SEPETU ASWEKWA NDANI HADI JUNI 24

WEMA SEPETU ASWEKWA NDANI HADI JUNI 24


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, imemwamuru msanii wa filamu nchini na Miss Tanzania wa mwaka 2006, Wema Sepetu,  kukaa mahabusu kwa siku saba hadi Jumatatu ijayo, Juni 24, wakati akisubiri uamuzi wa mahakama kumfutia dhamana baada ya kukiuka masharti aliyopewa mahakamani hapo.

Wema anakabiliwa na mashtaka ya kujipiga video ya ngono na kuisambaza katika mtandao wa kijamii wa Instagram.

SOMA NA HII  MBWANA SAMATTA AWASILI LEO