BEKI wa zamani wa Simba ambaye kwa sasa anakipiga timu ya FC Baroka ya Afrika Kusini leo amekutana na wachezaji wa Simba pamoja na viongozi ambao wametua timu Afrika Kusini kuweka kambi.
Beki huyo ameongeza furaha kwa wachezaji na viongozi wa Simba baada ya kuonana na kupiga picha ya kumbukumbu
Simba imeamua kuweka kambi ya muda wa wiki mbili nchini Afrika Kusini kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao unaotarajiwa kuanza Agosti 23 na mchezo wa kwanza itamenyana na JKT Tanzania.