Home Uncategorized AZAM FC: TUNALITAKA KOMBE LETU, MANYEMA SIRI ZAO TUNAZO

AZAM FC: TUNALITAKA KOMBE LETU, MANYEMA SIRI ZAO TUNAZO


KOCHA Msaidizi wa Azam FC, Idd Cheche amesema kuwa leo watapambana na Manyema FC ili kutinga hatua ya fainali kombe la Kagame na kuteta kombe lao.

Azam FC leo itamenyana na Manyema FC ya Congo kwenye hatua ya nusu fainali itakayochezwa nchini Rwanda.

Akizungumza na Saleh Jembe, Cheche amesema kuwa wanawatambua wapinzani wao vema kwa kuwa waliwashuhudia wakicheza na APR mchezo wa hatua ya robo fainali.

“Mbinu zao tunazajiua na namna wanavyofanya tunatambua hivyo tutapambana kupata matokeo chanya yatakayotusaidia kutetea kombe letu,” amesema.

SOMA NA HII  AZAM MEDIA YABORESHA HUDUMA,YAZINDUA KISIMBUSI CHA DIGITAL