MABINGWA watetezi wa kombe la Kagame Azam FC leo wameelekea nchini Rwanda na ndege ya Shirika la RwandaAir, ili kutetea taji lao.
Michuano hiyo inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Rwanda kuanzia Julai 6-21 mwaka huu.
Azam FC itamenyana na KCCA ya Uganda, Mukura ya Rwanda na Bandari ya Kenya.