Home Uncategorized DILI LA AFRIKA KUSINI LAWA GUMU KWA DIDA WA SIMBA

DILI LA AFRIKA KUSINI LAWA GUMU KWA DIDA WA SIMBA


DEOGRATIUS Munish ambaye ameachana na Simba baada ya kumaliza kandarasi yake ya mwaka mmoja amesema kuwa kwa sasa bado hajajua ni timu gani ataichezea kutokana na mipango kutokamilika.

Dida ambaye alisajiliwa na Simba akitokea timu ya Amatuks ya Afrika Kusini alikuwa na mpango wa kurejea huko ila kwa sasa amesema mambo hayajakaa sawa.

“Bado sijajua nitachezea timu gani msimu ujao kwani kwa sasa bado mambo yangu na timu ya Afrika Kusini hayajakaa sawa,ila muda ukitimia kila kitu kitakuwa sawa,” amesema. Dida.

SOMA NA HII  BREAKING: AMUNIKE APIGWA CHINI STARS, MBADALA WAKE AANZA KUSAKWA