Home Uncategorized HAJI MANARA APEWA JUKUMU JIPYA NDANI YA SIMBA

HAJI MANARA APEWA JUKUMU JIPYA NDANI YA SIMBA



UONGOZI wa Simba umesema kuwa umempa kazi maalumu Ofisa Habari wa kikosi hicho kabla ya siku ya Simba day ambayo ni maalumu kwa ajili ya kutambulisha wachezaji na jezi za Simba.


Mtendaji Mkuu wa Simba, Crescentius Magori amesema kuwa mpango wao ni kuona wanaifanya siku hiyo kiupekee.

“Simba day ya mwaka huu itakuwa tofauti na nyingine hivyo Haji Manara amepewa kazi maalumu kwa ajili ya kuandaa wimbo maalumu utakaotumika siku hiyo hivyo mashabiki waendelee kutupa sapoti,” amesema.
SOMA NA HII  TAKUKURU YABAINISHA KINACHOENDELEA ISHU YA BILIONI MOJA YA MAGUFULI KWA AJILI YA AFCON