Home Uncategorized KMC: TUPO TAYARI KUPAMBANA KIMATAIFA

KMC: TUPO TAYARI KUPAMBANA KIMATAIFA

UONGOZI wa KMC umesema kuwa hauna mashaka na kikosi walichopangiwa nacho kucheza nao kwenye michuano ya kimataifa kwani wana uwezo wa kufanya maajabu.

Ofisa Habari wa KMC, Anwari Binde amesema kuwa tayari wameanza maandalizi kwa ajili ya michuano ya kimataifa wana imani ya kufanya vizuri.

“Tumefurahi kuona kwamba tunaanzia Rwanda na AS Kigali, tumeshiriki michuano ya Kagame hivyo tunauzoefu na timu za Rwanda, tumeweza kumfunga bingwa Rayon Sports hivyo tualeta ushindani,” amesema.

KMC itamenyana na AS Kigali kati ya Agosti 9/11 mchezo wa kombe la Shirikisho nchini Rwanda kabla ya kurudiana Agosti 23 au 25.

SOMA NA HII  KAZE KUONGEZA MAJEMBE MENGINE NDANI YA KIKOSI CHA YANGA