Home Uncategorized AZAM FC KUTESTI MITAMBO KWA NAMUNGO FC LEO

AZAM FC KUTESTI MITAMBO KWA NAMUNGO FC LEO

KIKOSI cha Azam FC leo kitacheza mchezo wa kirafiki na Namungo FC uwanja wa Chamazi majira ya saa 1:00 jioni.

Mchezo huo wa kirafiki ni maalumu kwa ajili ya maandalizi ya michezo yake miwili iliyopo mkononi ambayo ni ule dhidi ya Simba, Jumamosi pamoja na Fasil Kenema ya Ethiopia.

Azam ana kibarua cha kucheza na Simba Jumamosi, Uwanja wa Taifa mchezo wa ngao ya jamii na kati ya Agosti 23-25 atacheza na Fasil Kenema ya Ethiopia mchezo wa marudio wa kombe la Shirikisho Afrika.

SOMA NA HII  NAHODHA WA REAL MADRID AWATAKA WACHEZAJI KUJIKOSOA ILI KUTWAA UBINGWA WA LA LIGA