Home Uncategorized MANCHESTER CITY: MSIMU UJAO KAZI ITAKUWA NGUMU ILA IMANI IPO

MANCHESTER CITY: MSIMU UJAO KAZI ITAKUWA NGUMU ILA IMANI IPO


PEP Guardiola, Meneja wa Manchester City, amesema kuwa kwa sasa wameanza na mwanzo mzuri hasa baada ya kutwaa taji la ngao ya jamii.

Manchester City ni mabingwa watetezi wa kombe la Ligi Kuu ya England ambalo walitwaa msimu uliopita baada ya kufikisha pointi 98 wakiwaacha wapinzani wao Liverpool kwa pointi moja.

Guardiola amesema kuwa:’ Tumeanza vizuri hivyo ni muda wetu wa kuendeleza rekodi zetu ambazo tumeziona kwani kushinda kombe mwanzo kutawafanya wachezaji wacheze kwa kujituma zaidi.

“Natambua kwamba msimu ujao ushindani utakuwa mkubwa ila tupo tayari kwani maandalizi yamekuwa mazuri kwetu,” amesema.

SOMA NA HII  KAGERA SUGAR MAJANGA MATUPU, DAKIKA 270 BILA POINTI KIBINDONI