Home Uncategorized YANGA: KWA MOTO WA SIBOMANA, BALINYA LAZIMA KARIOBANG SHARK WAKAE

YANGA: KWA MOTO WA SIBOMANA, BALINYA LAZIMA KARIOBANG SHARK WAKAE

DEO Muta, Katibu wa Kamati ya Hamasa ndani ya Yanga amesema kuwa hakuna namna itakayowazuia wapinzani wao Kariobang Sharks Kupata ushindi mbele ya Yanga.

Muta amesema kuwa Yanga imejipanga kufanya makubwa na maajabu hivyo mashabiki wajitokeze kwa wingi.

“Kilele cha Mwananchi ni moto wa kuotea mbali kikosi chetu ni imara na ni lazima tuwanyooshe hao Kariobang Sharks hivyo mashabiki wajitokeze kwa wingi uhakika upo kwani kikosi ni imara,” amesema.

Yanga ina wachezaji nyota kama Patrick Sibomana, Juma Balinya, Mrisho Ngassa, Papy Tshishimbi ambao wataongoza kikosi siku ya kilele cha Mwananchi Agosti 4 uwanja wa Taifa.

SOMA NA HII  BEKI MZAWA DAVID LUHENDE AINGIA ANGA ZA SIMBA NA YANGA