Home Uncategorized ZAHERA AJA NA RIPOTI YA BOXER YANGA, ATUMIA VIDEO KUWAFUATILIA ROLLERS

ZAHERA AJA NA RIPOTI YA BOXER YANGA, ATUMIA VIDEO KUWAFUATILIA ROLLERS


Kocha Mkuu wa Yanga, Mwinyi Zahera amesema wachezaji wa kikosi chake wako vizuri tayari kwa mechi za kitafiki kuelekea Mchezo wa marudiano wa klabu Bingwa Afrika dhidi ya Township Rollers ya Botswana.

Amesema tayari wachezaji Kelvin Yondani na Juma Abdul wameingia kikosini na kwamba beki Paul Godfrey ‘Boxer’ anaeendelea vyema muda wowote anaweza kujiunga na wenzake kikosini.

Amesema wanaendelea kuwasoma wapinzani wao kwa kupitia video zao mbalimbali ili kujua namna ya kucheza nao na kupata ushindi katika Mchezo wa marudiano.

SOMA NA HII  AUSSEMS AWAPIGA MKWARA WACHEZAJI WAWILI SIMBA