Home Uncategorized AUSSEMS APOTEZWA SIMBA

AUSSEMS APOTEZWA SIMBA


Sven Vanderbroeck, Kocha Mkuu wa Simba ameipoteza rekodi ya mtangulizi wake, Patrick Aussems kwenye mechi za Kanda ya Ziwa kwa kusepa na idadi kubwa ya pointi na mabao.

Simba msimu wa 2018/19, chini ya Aussems kwenye mechi mbili za kanda ya ziwa, mkoani Mwanza iliambulia pointi tatu na mabao mawili huku ikifungwa bao 1-0 na Mbao FC Uwanja wa Kirumba na ilishinda kwa mabao 2-0 mbele ya Alliance FC.

Msimu wa 2019/20, Sven amefungwa mabao mawili na amejikusanyia jumla ya mabao sita alianza kushinda mabao 2-1 mbele ya Mbao FC na mbele ya Alliance FC alishinda mabao 4-1 na kumfanya arudi Dar akiwa na jumla ya pointi sita kibindoni.

Ushindi huo unaifanya Simba ikusanye jumla ya pointi 41 ikiwa imecheza mechi 16 ipo nafasi ya kwanza tofauti ya pointi 16 na watani zao wa jadi Yanga wenye pointi 25, nafasi ya nane na wamecheza mechi 14.
SOMA NA HII  NEEMA KUBWA KINOMA YAWAANGUKIA YANGA