Home Uncategorized MBELGIJI WA YANGA NA MSAUZI WAPEWA MWAKA MMOJA NA MIEZI SITA

MBELGIJI WA YANGA NA MSAUZI WAPEWA MWAKA MMOJA NA MIEZI SITA


LUC Eymael Kocha Mkuuwa Yanga, raia wa Ubelgiji na Riedoh Berdien, Kocha Msaidizi na viungo wameingia mkataba wa mwaka mmoja na miezi sita kuitumikia Yanga.

Eymael amejiunga na Yanga akichukua mikoba ya Mwinyi Zahera ambaye alitimuliwa ndani ya kikosi hicho kutokana na kuwa na matokeo mabovu ndani ya Yanga.

Leo, Mbelgiji huyo alianza kazi na kikosi chake hicho kinachojiaanda kumenyana na Kagera Sugar, Jumatano mchezo wa ligi.

SOMA NA HII  MANARA AIBUKA NA KALI NYINGINE JUU YA TAIFA STARS - VIDEO