Home Uncategorized JOSE MOURINHO AANZA MIKWARA YAKE KWA NYOTA WAKE MPYA SASA

JOSE MOURINHO AANZA MIKWARA YAKE KWA NYOTA WAKE MPYA SASA


JOSE Mourinho, Kocha Mkuu wa Spurs amesema kuwa anaamini nyota wake mpya Steven Bergwijn ataonyesha makubwa mbele ndani ya timu yake.

Raia huyo wa Netherlands aliyekuwa akikipiga PSV Eindhoven alifunga bao lake la kwanza akiwa na timu yake ya Spurs mbele ya Manchester City kwenye mchezo wa Ligi Kuu England.

Mourinho amesema kuwa hakuna haja ya kujiuliza maswali mengi juu ya kijana huyo ana amini ataonyesha kazi kubwa ndani ya Uwanja.

Bao la kwanza alifunga Bergwijin dakika ya 63 na la pili lilifungwa na Son Heung-Min dakika ya 71 na kuwafanya Spurs kufikisha jumla ya pointi 37 nafasi ya tano huku City wakiwa na pointi 51 nafasi ya pili.

SOMA NA HII  MUUAJI WA SIMBA APEWA JUKUMU LINGINE LA KUIMALIZA KWA MARA NYINGINE TENA TAIFA

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here