Home Uncategorized KUMBE! UGUMU WA LIGI WAIPA PRESHA JKT TANZANIA

KUMBE! UGUMU WA LIGI WAIPA PRESHA JKT TANZANIA


ABDALLAH Mohamed ‘Bares’, Kocha Mkuu wa JKT Tanzania amesema kuwa ugumu wa Ligi Kuu Bara unawafanya wachezaji wake wajitume uwanjani jambo analoamini kwamba wataibuka washindi kwenye mchezo wao dhidi ya Biashara United.

Uwanja wa Jamhuri, Dodoma leo Februari, 18,2020 utashuhudia miguu 22 ya wanaume wakisaka pointi tatu muhimu.

Bares amesema:”Ligi ni ngumu na kila timu inapambana kupata matokeo, vijana wangu wapo tayari kwa ushindani nina amini tutapata pointi tatu ili kuzidi kuwa kwenye nafasi bora zaidi,”.

JKT Tanzania kwenye msimamo ipo nafasi ya saba na ina pointi 34 huku Biashara United ikiwa nafasi ya 9 na pointi 31.

SOMA NA HII  MUONEKANO WA UKURASA WA NYUMA GAZETI LA CHAMPIONI IJUMAA

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here