Home Uncategorized SIMBA : WAPINZANI WETU WALIKUWA VIZURI, TULISHINDWA KUTUMIA NAFASI

SIMBA : WAPINZANI WETU WALIKUWA VIZURI, TULISHINDWA KUTUMIA NAFASI

JOHN Bocco, nahodha wa Simba amesema kuwa kilichowaponza washindwe kupata matokeo mbele ya JKT Tanzania, Uwanja wa Uhuru ni kushindwa kutumia nafasi walizozipata.

Simba ilichapwa bao 1-0 mbele ya JKT Tanzania kwenye mchezo wa kwanza wa mzunguko wa pili. Bao pekee la ushindi lilifungwa na mshambuliaji Adam Adam dakika ya 24.

Bocco amesema: “Mchezo ulikuwa mgumu na wapinzani wetu walikuwa vizuri, wametengeneza nafasi moja nasi tumetengeneza nafasi tumeshindwa kuzitumia.

“Kikubwa tunashukuru kwa kuwa mchezo tumemaliza salama, tunachokifanya kwa sasa ni kujipanga kwa ajili ya mechi zetu nyingine,”.

Mchezo wa kwanza wa mzunguko wa kwanza, Simba ilishinda kwa mabao 3-1, jana, Februari 7, JKT Tanzania ililipa kisasi na kusepa na pointi tatu jumla.

SOMA NA HII  CHEKI PICHA PICHA SOSO AKIUAGA UKAPERA