Home Uncategorized ALLIANCE YAKWAMA KUFUTA UTEJA MBELE YA AZAM FC

ALLIANCE YAKWAMA KUFUTA UTEJA MBELE YA AZAM FC

AZAM FC jana imeinyoosha Alliance FC ya Fred Minziro kwa ushindi wa bao 1-0.

Mchezo huo uliochezwa Uwanja wa Uhuru ulikuwa na ushindani mkubwa ambapo Alliance walikuwa wakipambana 
kufuta uteja mbele ya Azam FC.

Kwenye mchezo wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Nyamgana, Azam FC  iliinyoosha mabao 5-0 Alliance jambo lililokuwa likiwatesa Alliance.

Bao pekee la ushindi kwa Azam FC lilifungwa na Frank Domayo baada ya mlinda mlango wa Alliance kuutema mpira akiwa ndani ya 18.

SOMA NA HII  BEKI HUYU CHIPUKIZI AINGIA ANGA ZA SIMBA