Home Uncategorized SABABU ILIYOMFANYA CHAMA AKATUA SIMBA HII HAPA

SABABU ILIYOMFANYA CHAMA AKATUA SIMBA HII HAPA

CLATOUS Chama nyota anayekipiga ndani ya Simba amesema kuwa sababu kubwa iliyomfanya akubali kujiunga na klabu hiyo ni malengo ambayo aliyaona kwa mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Chama alijiunga na Simba msimu wa 2018/19 akitokea Klabu ya Power Dynamo ya Zambia na msimu wake wa kwanza alitwaa Kombe la Ligi Kuu Bara na kufika hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Chama amesema:”Sababu kubwa iliyonifanya nikakubali kujiunga na Simba ni mipango ambayo niliona wanayo ilikuwa bora na walikuwa na kiu ya kufika mbali kimataifa.

“Hilo lililitokea msimu uliopita ambapo tulifika hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika ila ni hatua nzuri kwetu na sehemu ya kujivunia kwa kufanya hivyo,”.

SOMA NA HII  BREAKING:GWIJI MARADONA AFARIKI DUNIA

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here