Home Uncategorized COASTAL UNION HAINA MPANGO WA KUBORESHA KIKOSI CHAO

COASTAL UNION HAINA MPANGO WA KUBORESHA KIKOSI CHAO

JUMA Mgunda,Kocha Mkuu wa Coastal Union amesema kuwa kwa sasa hafikirii kuhusu masuala ya usajili.

 Mgunda ni miongoni mwa makocha wazawa ambao wanafanya vizuri kwa sasa ndani ya Bongo amekiongoza kikosi chake cha Coatal Union kwenye mechi 28 na kimejikusanyia jumla ya pointi 46 kikiwa nafasi ya tano.

Mgunda amesema:- “Masuala ya kufikiria kuboresha kikosi kwa sasa wakati kuna janga la Virusi vya Corona hakuna kabisa mpango huo.

“Ninaamini kuwa kikosi changu bado kipo imara na bora iwapo kuna sehemu ya kuboresha tutafanya hivyo wakati ukifika,” .

Ligi Kuu Bara ilisimamishwa Machi 17 na Serikali kutokana na maambukizi ya Virusi vya Corona ambavyo vinaitikisa dunia.

SOMA NA HII  WAWILI KUPIGWA PANGA NDANI YA AZAM FC MAZIMA