Home Uncategorized ISHU YA LIGI KUU BARA KUREJEA, SIMBA YATOA TAMKO

ISHU YA LIGI KUU BARA KUREJEA, SIMBA YATOA TAMKO

UONGOZI wa Simba umesema kuwa baada ya Ligi Kuu Bara kutangazwa tarhe ya kurejea na Serikali ambayo ni Juni Mosi itaendeleza rekodi ya kubeba taji la ligi mfululizo.

Jana, Mei 22, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufli alisema kuwa kutokana na maabukizi ya Virusi vya Corona kupungua ni ruksa kwa masuala ya michezo kuendelea kuanzia Juni Mosi.

Masuala ya mikusanyiko isiyo ya lazima ilisimamishwa Machi 17 baada ya janga la Corona kuivurugavuruga dunia.


Ofisa Habari wa Simba Haji Manara amesema kuwa kwa kuwa tayari Magufuli amesharuhusu ligi kuendelea hesabu zao za kutwaa makombe zitaendelea.

“Simba itachukua back 2 back kumi mfululizo, tunajiamini kwa kuwa tuna kikosi imara na wachezaji wazuri basi tusubiri na tuone,”.

SOMA NA HII  MBABE WA YANGA HAPOI AIBUKIA HUKU