Home Uncategorized POLISI TANZANIA WAKIWA KAZINI BADO WANATAMBUA UWEPO WA CORONA

POLISI TANZANIA WAKIWA KAZINI BADO WANATAMBUA UWEPO WA CORONA


TIMU ya Polisi Tanzania iliyo chini ya Kocha Mkuu, Malale Hamsini inaendelea kuchukua tahadhari dhidi ya Virusi vya Corona.

Polisi Tanzania tayari imeanza mazoezi yake kujiaanda na mechi za kumaliza msimu wa 2019/20.

Ofisa Habari wa Polisi Tanzania, Frank Lukwaro amesema kuwa wameanza mazoezi ili kujiaandaa mapema huku wakiendelea kuchukua tahadhari dhidi ya Virusi vya Corona.

“Bado tunaendelea kufuata utaratibu uliowekwa na Wizara ya Afya pamoja na Serikali katika kujilinda na Corona na tumeanza mazoezi mapema ili kujiweka sawa kwani ushindani sio mchezo,”.

Masuala ya michezo yalisimamishwa Machi 17 na Serikali kutokana na janga la Virusi vya Corona tayari Serikali imeruhusu masuala ya michezo kuanza ifikapo Juni Mosi.

SOMA NA HII  KMC YAZITAKA POINTI TATU ZA VINARA WA LIGI AZAM FC

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here