ANAANDIKA Saleh Jembe kuhusu maoni masuala ya nembe ndani ya Klabu ya Yanga namna hii:-Nimezungumza mara nyingi sana kuhusiana na hili suala lakini WASIO NA HOJA akaishia kwenye Matusi, sasa leo TUJIFUNZE TENA.
ANGALIA LOGO ya Sevilla FC ina rangi nyingi nyekundu na leo Yanga wanaingia nao mkataba logo yao ikiwa na rangi zake.
Hapa nyumbani kampuni zote zilizoingia mkataba na Yanga kwa maana ya kuwa zinatoa fedha, bado Yanga walishindwa kuonyesha heshima na baadaye kulazimika kubadili rangi za logo zao.
Mfano mzuri, wadhamini wa ligi Vodacom ambao Yanga wanafaidika nao… Angalia GSM PIA.
Utasikia sisi hatuwezi kufanya kazi na watu wenye rangi nyekundu.
Nimefafanua mara nyingi sana kuwa si kila nyekundu ni Simba au kila njano ni Yanga.
Wadhamini au partners wanapaswa KUHESHIMIWA na vizuri tukaacha “USHAMBA WA RANGI”… Hili la Sevilla na La Liga linaweza kuwa funzo kwa wale ambao kweli hawakuwa wakielewa au wale walikuwa HAWAELEWI KWA MAKUSUDI..
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.