Home Uncategorized KESHO YANGA V AZAM NI BALAA, DATA NI NOMA

KESHO YANGA V AZAM NI BALAA, DATA NI NOMA


KESHO Uwanja wa Taifa wanaume 22 miguu yao itapambana kusaka pointi tatu ndani ya Ligi Kuu Bara.

Kwa mujibu wa takwimu hizo, Azam FC imekutana na Yanga mara 23 kwenye mechi za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL).

Azam FC imeshinda mara nane kama ilivyo kwa Yanga, zikatoka sare mara saba, huku wababe hao wa Chamazi wakifunga jumla ya mabao 31 na Yanga wakitupia 30.

Mchezo wa kesho Jumapili, utakuwa na ushindani mkubwa hasa ukizingatia kila timu inawania nafasi ya pili kwenye msimamo, zikipishana pointi mbili, Azam FC ikiwa imejikusanyia pointi 57 katika nafasi hiyo huku Yanga ikiwa nazo 55.

SOMA NA HII  CHAMA AKUBALI MUZIKI WA TIMU YAKE YA SIMBA