Home Uncategorized KOCHA YANGA ATUA DAR KUMALIZANA NA MABOSI WAKE

KOCHA YANGA ATUA DAR KUMALIZANA NA MABOSI WAKE

 

ZLATKO Krmpotic Kocha Mkuu wa Yanga amewasili leo Agosti 29 Dar es Salaam kwa ajili ya kuanza kukinoa kikosi hicho ambacho kilianza mazoezi Agosti 10.
Raia huyo wa Serbia anachukua mikoba ya Luc Eymael ambaye alifutwa kazi Julai 27 baada ya kutoa lugha za kiubaguzi.

Anaungana na Juma Mwambusi ambaye ni kocha msaidizi tayari alishaanza kazi ya kukinoa kikosi hicho Uwanja wa Chuo cha Sheria.

Zlatko amepewa kandarasi ya miaka miwili kukinoa kikosi hicho chenye maskani yake Jangwani na kwa sasa kinajiandaa kwa ajili ya Wiki ya Mwananchi ambapo kilele chake ni kesho Agosti 30, Uwanja wa Mkapa,
Siku hiyo ni rasmi kwa ajili ya kutambulisha wachezaji wapya na wale ambao walikuwa na kikosi kwa msimu wa 2019/20.
SOMA NA HII  NIYONZIMA WA SIMBA KUIBUKIA CONGO

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here