Home Uncategorized HIZI HAPA 12 LEO KUANZA KUSAKA POINTI TATU NDANI YA LIGI KUU...

HIZI HAPA 12 LEO KUANZA KUSAKA POINTI TATU NDANI YA LIGI KUU BARA

 

LEO Septemba 6 mitambo ndani ya Ligi Kuu Tanzania Bara inawashwa rasmi ambapo timu 12 zitakuwa kwenye viwanja vitano kusaka pointi tatu muhimu na kesho sita zitakuwa kazini kukamilisha mzunguko wa kwanza.

Mabingwa watetezi wa ligi ni Simba wao watakuwa ugenini, Mbeya kumenyana na Ihefu FC, Uwanja wa Sokoine huku watani zao wa jadi, Yanga wakiwa pale Uwanja wa Mkapa kumenyana na Tanzania Prisons.

Namungo FC iliyo chini ya Kocha Mkuu, Hitimana Thiery itamkaribisha Juma Mgunda wa Coastal Union Uwanja wa Majaliwa.Biashara United itaanza na Gwambina FC, Uwanja wa Karume huku Dodoma Jiji ikimenyana na Mwadui FC, Uwanja wa Jamhuri, Dodoma.

Mtibwa Sugar itamalizana na wanajeshi Ruvu Shooting, Uwanja wa Gairo, Morogoro.Mechi zote zinatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kwa kuwa timu zote zinahitaji kutwaa taji la Ligi Kuu Bara.

SOMA NA HII  YANGA WATOA TAMKO JINGINE JUU YA NDEMLA NA MKUDE