Home Uncategorized KOCHA SIMBA ATAJA SABABU YA WACHEZAJI WAKE KUJENGA USHKAJI NA BENCHI

KOCHA SIMBA ATAJA SABABU YA WACHEZAJI WAKE KUJENGA USHKAJI NA BENCHI


 KOCHA Mkuu wa Simba, Sven Vandenbroeck amesema kuwa haijalishi ni mchezaji wa aina gani ambaye yupo kwenye kikosi chake wote ni sawa na wana nafasi ya kuanzia benchi pamoja na kikosi cha kwanza.


Miongoni mwa wachezaji ambao walikuwa na uhakika wa namba kikosi cha kwanza msimu ulipota wa 2019/20 ni pamoja na Meddie Kagere ambaye ni mfungaji bora wa misimu miwili mfululizo akiwa amefunga jumla ya mabao 45, Erasto Nyoni ambaye msimu uliopita alifunga bao moja, Pascal Wawa ambaye alitoa jumla ya pasi moja kati ya mabao 78 waliyofunga Simba.


Kwa sasa Simba inajiwinda na mchezo wake dhidi ya Biashara United unaotarajiwa kuchezwa Septemba 20, Uwanja wa Mkapa ambapo wachezaji walikuwa na mchezo dhidi ya Biashara United.


Sven amesema:”Haijalishi mchezaji ni ana uwezo wa kufunga ama ana tuzo ya mfungaji bora, ndani ya Sima wachezaji wote ni sawa na kila mchezaji ana hitaji kucheza na ana nafasi ya kukaa benchi kikubwa tunahitaji ushindi.”


Kwenye mechi mbili za ligi, Kagere ametumia jumla ya dakika 47, alitumia dakika 23 kwenye mchezo dhidi ya Ihefu kisha akatumia dakika 24 mbele ya Mtibwa Sugar.


Wawa na Nyoni ambao ni mabeki visiki ndani ya Simba hawajapata nafasi ya kutumia dakika hata moja ndani ya mechi mbili za ligi.

SOMA NA HII  CHEKI NAMNA MAKUNDI YA AFCON MWAKA 2021 YALIVYO, TANZANIA SAHANI MOJA NA WAARABU

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here