SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limetoa tamko likikemea kitendo cha mashabiki wa Yanga SC kuwafanyia fujo mashabiki wa Simba SC katika Uwanja wa Jamhuri Morogoro kwenye mchezo wa Yanga vs Mtibwa Sugar uliofanyika jana Jumapili, Septemba 27, 2020.
Kwenye mchezo huo Mtibwa Sugar ilipoteza kwa kufungwa bao 1-0 lililopachikwa na beki Lamine Moro dakika ya 61.