Home Uncategorized BALOZI WA TANZANIA AITEMBELEA KAMBI YA SIMBA NIGERIA

BALOZI WA TANZANIA AITEMBELEA KAMBI YA SIMBA NIGERIA


BALOZI wa Tanzania nchini Nigeria Benson Bana ametembelea kambi ya Simba jijini Abuja na kupewa jezi ya Simba itakayotumika Kwenye mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika. 


Simba Novemba 29 itamenyana na Plateau United mchezo wa awali wa Ligi ya Mabingwa Afrika


Kiongozi huyo amesema kuwa ana imani ya kuona timu ya Simba ikipata matokeo chanya Kwenye mchezo huo ambao unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.


Mratibu wa Simba, Abbas Ally amesema kuwa maandalizi yapo sawa na wachezaji wapo tayari kwa mchezo huo kabla ya ule wa marudio utakaochezwa Dar.

SOMA NA HII  MWINYI ZAHERA: MOLINGA AMEPONZWA NA BENCHI NDIO MAANA HAJAFUNGA MABAO 15