Home Uncategorized KISINDA KUFANYIWA VIPIMO ZAIDI ILI KUPATA MATIBABU

KISINDA KUFANYIWA VIPIMO ZAIDI ILI KUPATA MATIBABU

 


NYOTA wa Yanga, Tuisila Kisindaatafanyiwa vipimo zaidi ili kujua ukubwa wa tatizo pamoja na kupewa matibabu bora yatakayomrejesha uwanja kuendelea na kazi.


 Kwenye mchezo wa janan, Desemba 12 Uwanja wa Kambarage wakati Yanga ikishinda mabao 5-0 Kisinda alipata majeraha ya goti la mguu wa kushoto na alishindwa kuamaliza dakika 90.

 Kwa sasa inasubiriwa ripoti kutoka kwa daktari ili kujua tatizo lilivyo ili apewe matibabu haraka yatakayomrejesha kwenye kazi yake ya kutimiza majukumu ndani ya Yanga inayonolewa na Cedric Kaze.

Kwenye mchezo wa jana, Kisinda alifunga bao moja kwa pasi ya Yacouba Sogne dakika ya 56 na kuifanya timu hiyo kusepa na pointi tatu jumla.

Kaze amesema kuwa baada ya ripoti watajua ni muda gani mchezaji huyo atakuwa nje ya uwanja kwa matibabu kwa kuwa ripoti bado haijatoka. 
SOMA NA HII  KIKOSI CHA SIMBA KITAKACHOANZA LEO DHIDI YA IHEFU FC,MORRISON NDANI