Home Uncategorized NIYONZIMA:TUTACHUKUA UBINGWA WA LIGI KUU BARA

NIYONZIMA:TUTACHUKUA UBINGWA WA LIGI KUU BARA

 


BAADA ya kusaini dili la mwaka mmoja kiungo fundi wa kuchezea mpira, Haruna Niyonzima amesema kuwa anaamini timu hiyo itatwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara. 


Yanga ipo nafasi ya kwanza ikiwa na pointi 37 baada ya kucheza jumla ya mechi 15.


Imeshinda mechi 11, sare nne na haijapoteza mchezo, ikiwa imefunga mabao 22, Niyonzima amefunga bao ilikuwa ni Uwanja wa Mkapa wakati Yanga ikishinda mabao 3-0.


Niyonzima ameongeza mkataba wa mwaka mmoja ndani ya Yanga hivyo ataendelea kupambana mbele ya Kocha Mkuu,  Cedric Kaze. 


Nyota huyo amesema:”Nipo Yanga kwa sasa na ninafuraha kubwa, imani yangu ni kuona kwamba tunatimiza malengo tuliyojiwekea ili kufikia malengo tuliyojiwekea.


“Tunahitaji ubingwa na hilo lipo wazi, tunaamini kwamba tutafikia malengo hayo,” .

SOMA NA HII  BEKI IHEFU FC NJE YA UWANJA WIKI NNE

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here