Home Simba SC CHIKWENDE AAHIDI KUUPIGA MWINGI SIMBA

CHIKWENDE AAHIDI KUUPIGA MWINGI SIMBA

 


KIUNGO mshambuliaji mpya wa klabu ya Simba, Perfect Tatenda Chikwende amefunguka kuwa atahakikisha anacheza kwa kiwango kikubwa akiwa na jezi ya Simba ili kuisadia kufikia malengo waliyojiwekea msimu huu.

Chikwende alitambulishwa rasmi na kikosi cha Simba usiku wa majira ya saa 5 na dakika 59 siku ya Ijumaa baada ya kukamilisha dili lake akitokea kwenye kikosi cha klabu ya FC Platinum ya kwao nchini Zimbabwe.

Chikwende alipata dili hilo baada ya kuonyesha uwezo mkubwa kwenye michezo miwili ya Ligi ya mabingwa Afrika waliyocheza dhidi ya Simba amnbayo Simba walishinda kwa mabao 4-1 huku bao pekee la Platinum likiwekwa kambani na Mzimbabwe huyo.

Chikwende anakamilisha listi ya wachezaji wawili tua mbao Simba imewasajili katika usajili wa dirisha dogo lililofunguliwa rasmi Desema 16 na kufungwa usiku wa Ijumaa ya Januari 15.

Akizungumzia kuhusu kumwaga kwake wino ndani ya klabu ya Simba, Chikwende amesema: “Nimejiunga na Simba nikijua wazi kuwa hii ni miongoni mwa klabu kubwa, na naahidi kujituma kwa uwezo wangu wote ili kuisaidia kufikia malengo yake,”

SOMA NA HII  SOPU AZIGONGANISHA SIMBA NA YANGA....MMOJA AANZA MAZUNGUMZO NAYE...MWINGINE AMPANDIA DAU JUU KWA JUU....