Home Taifa Stars KOCHA ZAMBIA ATOA KAULI YA KIBABE AKIIVAA TANZANIA

KOCHA ZAMBIA ATOA KAULI YA KIBABE AKIIVAA TANZANIA

KOCHA mkuu wa timu ya taifa ya Zambia, Sredojevic Milutin Micho amekiri kwamba anatarajia kukutana na mchezo mgumu dhidi ya Taifa Stars leo.

Zambia leo itacheza dhidi ya Taifa Stars kwenye mchezo wao wa kwanza wa kundi D la michuano ya CHAN, mchezo utakaopigwa jijini Limbe, Cameroon majira ya saa 1:00 jioni kwa saa za Afrika Mashariki.

Akizungumzia mchezo huo Micho amesema: “Tunaiheshimu Tanzania kwakuwa najua wana ligi ya ndani nzuri na imara, najua ubora wao mpaka kufikia hapa ila tumejiandaa kupambana nao leo hii,”

Hizi ni fainali za tatu kwa Micho ambaye amewahi kupita kwenye kikosi cha klabu ya Yanga, ambapo fainali mbili za kwanza alikuwa akikiongoza kikosi cha Uganda mwaka 2014 na 2016.

SOMA NA HII  STARS WATAJA SABABU YA KUPOTEZA MCHEZO MBELE YA EQUATORIAL GUINEA