Home kimataifa MO SALAH KINARA WA UTUPIAJI ENGLAND

MO SALAH KINARA WA UTUPIAJI ENGLAND

 KWENYE orodha ya watupiaji ndani ya Ligi Kuu England, Mohamed Salah anayecheza ndaniya Liverpool ni kinara akiwa nayo  mabao 15 na ana pasi tatu za mabao.

Ndani ya Liverpool ambao ni mabingwa watetezi wa Ligi Kuu England amecheza mechi 20 kwa msimu wa 2020/21.

Salah raia wa Misri ana wastani wa kufunga bao moja kila baada ya dakika 110 na amepiga jumla ya mashuti 51.

Harry Kane na Son Heung-min wanamfuatia wote wapo ndani ya Tottenham Hotspur na wamefunga mabao 12 kwa msimu wa 2020/21.


SOMA NA HII  MESSI ATAJWA KUIBUKIA PSG