Home Azam FC AZAM WATAMBA KUMALIZA UTEJA LEO

AZAM WATAMBA KUMALIZA UTEJA LEO


NAHODHA wa kikosi cha klabu ya Azam, Aggrey Morris amefunguka kuwa kikosi hiko kimejipanga vizuri kuhakikisha wanamaliza uteja wa kupata matokeo katika uwanja wa Kaitaba kwenye mchezo wao wa leo dhidi ya Kagera Sugar, inayonolewa na kocha, Mecky Maxime.

Azam Jumamosi iliyopita iliibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mbuni katika mchezo wa kombe la FA na kutinga hatua ya 16 bora, ambapo wamekiri kuwa ushindi huo umeongeza morali ya kupambana kuelekea mchezo wa leo dhidi ya Kagera Sugar.

Azam inakamatia nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi ikiwa tayari imecheza michezo 21, na kujikusanyia pointi 37.

Akizungumzia mchezo huo, Morris alisema: “Kwanza tunajua wazi kuwa tunakwenda kucheza mchezo mgumu dhidi ya Kagera Sugar, mara zote tumekuwa na wakati mgumu kupata ushindi kwenye uwanja wa Kaitaba.

“Lakini wakati huu tumejiandaa vizuri kuhakikisha tunaibuka na pointi tatu muhimu dhidi yao, na tutapambana kutekeleza maagizo ya benchi la ufundi ili kuhakikisha tunalifanikisha hilo,”

SOMA NA HII  DEAL DONE....MKANDARA AKAMILISHA SAFARI YAKE YA KUTUA AZAM FC....SASA MAMBO NI 'BULIBULI'....