Home epl HARRY KANE AOMBA KUSEPA TOTTENHAM

HARRY KANE AOMBA KUSEPA TOTTENHAM

 


HARRY Kane, mshambuliaji wa Tottenham anataka kuomba kuondoka kwenye kikosi hicho mwishoni mwa msimu huu.


Nyota huyo raia wa England amekuwa kwenye kiwango bora muda mwingi ila hana bahati ya kutwaa mataji ndani ya kikosi hicho.
Kane amesema kuwa anahitaji kuomba kuondoka kwenye kikosi hicho msimu huu ili akapate changaoto mpya.
Taarifa zinaeleza kuwa nyota huyo anataka kwenda kuwatumia Real Madrid ama PSG licha ya kwamba yeye mwenyewe hajaweka wazi suala hilo.

Nyota huyo mwenye miaka 27 mkataba wake na Tottenham unatarajiwa kumalizika mwaka 2024 kwa kuwa alisaini mkataba wa miaka sita 2018. 
SOMA NA HII  RASMI..SERIKALI UINGEREZA YACHUKUA UMILIKI WA CHELSEA...YAZUIA DILI LA KUUZWA..HAKUNA KUSAJILI MCHEZAJI..