Home Ligi Kuu BILIONI 225.6 ZA AZAM MEDIA ZILETE CHACHU YA MAFANIKIO KWENYE SOKA LETU

BILIONI 225.6 ZA AZAM MEDIA ZILETE CHACHU YA MAFANIKIO KWENYE SOKA LETU


 IPO wazi kuwa kwa sasa uwekezaji katika ulimwengu wa mpira unazidi kutanua wigo ambapo wengi wanapenda kuwekeza na kuona matokeo ambayo yatakuwa mazuri. 

Azam Media Limited imeshinda zabuni ya haki za matangazo ya urushaji wa mechi za Ligi Kuu Tanzania bara wenye thamani ya shilingi Bilioni 225.6.


Kiasi hicho ni kikubwa kuwahi kutolewa kwa udhamini wa michezo nchini Tanzania na hata nchi jirani za Afrika Mashariki na Kati.

Kwa mujibu wa mkataba wa miaka 10 uliosainiwa jijini Dar es Salaam, asilimia 67 ya pesa hizo itakwenda moja kwa moja kwa timu ambazo zinashiriki ligi hiyo.

Azam TV pia itakuwa ikitoa zawadi (bonus) kwa Bingwa wa Ligi Kuu Tsh milioni 500, timu zinazofuata katika msimamo mpaka nafasi ya 16 zitakuwa zikinufaika pia.

Serikali itanufaika kwa kupata shilingi bilioni 34.4 zikiwa ni ni kodi ya ongezeko la thamani VAT.


Kwa hatua hii ambayo ni kubwa ni muhimu kwa kila timu kuongeza juhudi katika kusaka matokeo pamoja na kuona namna gani zitakuwa kwenye ushindani.


Licha ya mkataba ambao wameingia nao kuwa ni wa gharama kubwa hapo kuna masuala ninatambua kwamba yanahitaji kufanyiwa maboresho hasa ukizingatia kwamba kila siku kunaibuka changamoto mpya.
Jambo la msingi kwa kila mmoja kutimiza wajibu wake na kufanya kazi kwa vitendo. Hongereni Azam tena kwa kurejea na uwekezaji mkubwa.
Wakati huu mmekuwa tofauti ambapo mpaka zile timu zinazoshiriki Ligi Daraja la Kwanza pale ambapo watacheza play off watapewa zawadi hakika ni uwekezaji mkubwa.

Kila la kheri katika kutimiza yale makubaliano yenu na imani yetu ni kwamba kutakuwa na ushindani mkubwa kwa kila timu.
SOMA NA HII  VITENGO IMARA VYA MASOKO BADO NI TATIZO KUBWA KATIKA KLABU ZETU