Home Yanga SC KAHATA AWAITA YANGA MEZANI KWA DAU LOLOTE LILE WALILONALO

KAHATA AWAITA YANGA MEZANI KWA DAU LOLOTE LILE WALILONALO


FRANCIS Kahata  amekuwa mchezaji wa kwanza kuaga ndani ya Simba na sasa yupo kwao Kenya, kwani tayari ameondoka baada ya kumalizana na mabosi wake.

Julai 2019, Simba ilimsajili Kahata akitokea Gor Mahia inayoshiriki Ligi Kuu Kenya (KPL) kwa mkataba wa miaka miwili ambao ulipaswa kumalizika mwezi ujao.

Kahata si mchezaji mbaya, lakini ushindani wa namba alioupata kutoka kwa kina Luis Miquissone, Rally Bwalya, Bernard Morrison, Clatous Chama na Hassan Dilunga, ulimweka katika wakati mgumu kikosini Simba.

Baadaye uongozi wa Simba uliamua kumuweka kando kwa kumuondoa kwenye kikosi cha kucheza mechi za Ligi Kuu Bara msimu huu na kumbakiza katika mashindano ya kimataifa, Ligi ya Mabingwa Afrika tu, ambako timu hiyo iliishia hatua ya robo fainali.

Nafasi yake kwenye mechi za ndani ilichukuliwa na Perfect Chikwende, raia wa Zimbabwe ambaye pia tangu afike ameshindwa kuonyesha kiwango chake kili-chotarajiwa.Mwanaspoti lilifanya mahojiano maalumu na mchezaji huyo baada ya kumalizana na Simba ikiwa ni siku chache kabla ya kurudi kwao ambapo alielezea mambo mbalimbali tangu ajiunge na Wekundu hao wa Msimbazi.

 MAFANIKIO NA CHANGAMOTO

Akiwa na timu hiyo, amekuwa miongoni mwa wachezaji waliopata mafanikio makubwa baada ya kushinda mataji kama Ligi Kuu Bara, Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) na kufika hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Anasema kama mchezaji licha ya kuchukua mataji hayo pia amekutana na changamoto nyingi ikiwamo kuumia na kumfanya akae nje ya uwanja kwa muda mrefu.

“Kama mchezaji utakutana na changamoto nyingi ikiwamo kuumia wakati ligi inaelekea ukingoni kwa msimu wa 2019/20 ambapo mpaka msimu mpya unaanza sikuwa nimepona vizuri na nilipopona nilianza vizuri ingawa mabadiliko yaliyofanyika miezi sita iliyopita yalichangia kutokuwa na msimu mzuri kwa mwaka wangu wa pili licha ya kupata tuzo ya mchezaji bora wa mwezi,” anasema Kahata.

MABADILIKO YA LESENI

Akiwa ametoka kwenye majeraha na kuanza kurejea kwenye ubora wake, ndipo mabadiliko ya leseni yalifanyika upande wake kwa kumtoa ligi ya ndani na kumuacha michuano ya kimataifa pekee.Anasema kitendo hicho kilifan-yika pasipo kushirikishwa lolote jambo ambalo lilimvuruga kisaikolojia.

 “Mabadiliko yaliyofanyika ni kuhusu leseni yangu, mabadiliko hayo niliyasikia mitandaoni miezi sita iliyopita nikiwa nyumbani (Kenya) ya kuwa nafaa kucheza Ligi ya Mabingwa tu kwa sababu namba ya wache-zaji wa kigeni ilizidi na niliporudi Tanzania nilimpigia simu wakala wangu kujua nini kinaendelea, baadaye alizungumza na viongozi halafu akaja kwangu kunipa sababu hiyo ya uwepo wa idadi kubwa ya wachezaji wa kigeni.”Anasema mabadiliko hayo akiwa kama mchezaji yalimkosesha nafasi ya kucheza huku wenzake wakiwa wanacheza mechi nyingi zilizowasaidia kuwa fiti.

SOMA NA HII  KIGOGO YANGA ALIA MASHABIKI KUDHULUMIWA NA WACHEZAJI....ISHU IKO HIVI...

 KUPOTEZA NAMBA HARAMBEE STARS

Kiungo huyu mara kadhaa amekuwa akiitwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa Kenya ‘Harambee Stars’, lakini kutokana na kutopata nafasi ya kucheza ndani ya Simba kumemfanya aondolewe kwenye kikosi hicho pia.

Kahata alikuwa kwenye kikosi cha Harambee Stars kilichocheza Fainali za Mataifa Afrika (AFCON) 2019 baada ya hapo akasajiliwa Simba.

Anasema kuwa kutopewa nafasi ya kucheza ndio sababu kubwa ya kutoitwa kwenye kikosi hicho kwani makocha wanaita wachezaji wanaocheza. “Mechi za Ligi ya Mabingwa kwa mwezi zilikuwa zinachezwa mbili tu na ikumbukwe kuwa kocha nae huwa na machaguo yake sio kila mechi utapangiwa, wenzangu walikuwa wanacheza mechi nyingine za ligi ya ndani na kuwafanya wawe fiti na waitwe timu za taifa.

“Makocha huangalia viwango vya wachezaji wanapocheza michuano mbalimbali ya timu zao, kwangu imekuwa vigumu kuitwa,” anasema na kuongeza kuwa; “Hata Kocha Gomes (Didier) alipoingia na kuanza kufundisha alishangaa sana alipokuta leseni yangu imebadilishwa, ananifahamu tangu nikiwa Gór Mahia na alinishauri nisivunjike moyo kwani anafahamu uwezo wangu na nilikuwa nafanya mazoezi ili nisimuangushe.”

 HATAMSAHAU MO DEWJI

Anasema licha ya kundoka Simba hatamsahau Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Mohamed ‘Mo’ Dewji katika misimu yake miwili aliyokuwa na timu hiyo. Anasema hatawasahau pia mashabiki wa soka wa Simba kwa mapenzi yao na kuwapa sapoti muda wote na popote wanapokwenda kucheza.

“Nawashukuru viongozi wa Simba chini ya Mo Dewji kwa kuniamini na kunipatia mkataba wa miaka miwili kamwe sitawasahau na mashabiki waliokuwa wanaacha kazi zao kuja kushangilia timu inapocheza jambo lililotupa hamasa ya kujituma ili kushinda mechi, wanafanya kazi kubwa sana sijawahi kuona sapoti kama hiyo labda zamani kwa mashabiki wa Gor Mahia.

Mashabiki wa ligi ya Kenya zamani walikuwa wanashangilia timu zao hususani wa Gor Mahia, kwa sasa Corona imerud-isha nyuma mpira kwa kiasi kikubwa, nitawakumbuka sana mashabiki.”

 MKATABA UMEISHA HIVI

Mkataba wake ulikuwa umalizike Julai 4, 2021 lakini baada ya kuambiwa hatakuwa sehemu ya kikosi msimu ujao aliona ni vyema aondoke tu. “Hakukuwa na mazungumzo ya kuongeza mkataba kwani Mtendaji Mkuu wa Simba, Barbara Gonzalez alinipigia simu na kuniambia hawataweza kuendelea kuwa na mkataba kati yangu na wao.

“Simba ni timu ambayo wameni-patia upana mzuri kwani kwa sasa ni moja ya timu kubwa barani Afrika wamefika hatua ya robo fainali pia wamefanikiwa kuifunga timu kama Al Ahly inayoogopwa kutokana na kutwaa ubingwa wa michuano hiyo mara nyingi, kiufupi nina furaha kuwa sehemu ya timu kubwa barani Afrika licha ya kuondoka.”