Home news VPL: SIMBA V YANGA, UWANJA WA MKAPA

VPL: SIMBA V YANGA, UWANJA WA MKAPA


MASHABIKI wa Simba v Yanga wamejitokeza kwa wingi leo Uwanja wa Mkapa kushuhudia dabi ya kukata na shoka ambayo iliyeyuka Mei 8.

Nyota wa Simba, Bernard Morrison leo anatarajia kuanza mchezo wake wa kwanza mbele ya mabosi wake wa zamani Yanga ambao bado waneleza kuwa mchezaji huyo ni wao na kesi yao ipo kwenye mahakama ya usuluhishi, (Cas).

Mchezo wa mzunguko wa kwanza alikosekana kwa kuwa alipigwa pini kutocheza mechi tatu na Shirikisho la Soka Tanzania, (TFF) kwa kosa la kuonekana akipigana na nahodha wa Ruvu Shooting, Juma Nyosso 

SOMA NA HII  YANGA WAAMUA AISEEE...WAPELEKA 'FULL KIKOSI' ALGERIA...MASTAA WOTE MPAKA MAJERUHI WAENDA...