Home KMC FC PAMOJA NA KUCHWA NA YANGA..FARUK SHIKHALO ARUDI BONGO NA KUSAINI DILI JIPYA

PAMOJA NA KUCHWA NA YANGA..FARUK SHIKHALO ARUDI BONGO NA KUSAINI DILI JIPYA


ALIYEKUWA kipa wa Yanga, Faruk Shikhalo amejiunga na klabu ya KMC kwa mkataba wa mwaka mmoja kuitumikia timu hiyo.

Mtu wa karibu na mchezaji huyo alithibitishia  kwamba Shikhalo amesaini mkataba huo na anatarajia kwenda kujiunga na wenzake kambini.

“Shikhalo ameshasaini na KMC, timu ipo Morogoro yeye anakamilisha baadhi ya vitu ili aende akajiunge na wenzake,” kilisema chanzo hicho.

Shikhalo anaenda kukutana na kipa mkongwe, Juma Kaseja ambaye amejihakikishia nafasi ya kuanza kwenye kikosi cha KMC.

Kipa huyo aliachana na Yanga baada ya kutoongezewa mkataba  yeye na mwenzake Metacha Mnata huku nafasi zao zikichukuliwa na Diarra Djigui na Erick Johola.

SOMA NA HII  BAADA YA SIMBA KUPATA MDHAMINI MPYA....BOSI SportPesa AIBUKA NA HAYA....ADAI WALIFURAHI KUACHANA NAO...