Home BIashara United BIASHARA UNITED KAZI BADO INAENDELEA

BIASHARA UNITED KAZI BADO INAENDELEA


 WANAJESHI wa Mpakani, Biashara United kwa sasa wanatamba baada ya kumaliza kazi ya dakika 180 kwenye mechi ya awali.

Biashara United iliibuka na ushindi wa bao 1-0 ilipokuwa ugenini dhidi ya DIKHIL na ule wa pili uliochezwa Uwanja wa Azam FC ilishinda mabao 2-0 yaliyofungwa na Ramadhan Chombo wengi wanapenda kumuita Redondo.

Kocha wa Biashara United Patrick Odhiambo amesema kuwa vijana wake wanastahili pongezi kwa kuwa walipambana bila kukata tamaa mwanzo mwisho.

“Wachezaji walikuwa katika hali nzuri na wamepambana kwa ajili ya kupata matokeo chanya na mwisho wa siku wamefanikiwa kupata kile ambacho wanakihitaji.

“Bado kuna kazi kubwa na tunahitaji kupata matokeo hivyo mashabiki wazidi kuwa pamoja nasi kila kitu kitakuwa sawa,” amesema.


SOMA NA HII  KUWANIA KUFUZU AFCON MWAKANI...MANARA ALAMBA SHAVU TIMU YA TAIFA YA BURUNDI...AIKANA YANGA....