Home news ALICHOSEMA MANARA KUHUSU MCHANGO WA RAIS SAMIA KWENYE MECHI YA JUZI…ATAJA MILION...

ALICHOSEMA MANARA KUHUSU MCHANGO WA RAIS SAMIA KWENYE MECHI YA JUZI…ATAJA MILION 41..


HAJI Manara, Ofisa Habari wa Yanga amesema kuwa kupitia mchezo wa Hisani kati ya Yanga vs Timu ya Taifa ya Somalia ni milioni 41 zimekusanywa.

Yanga ilicheza mchezo wa kirafiki wa hisani ilikuwa dhidi ya Timu ya Taifa ya Somalia ulichezwa Uwanja wa Azam Complex.

Manara amesema:”Mchezo uliochezwa Jumamosi iliyopita kwa ajili ya kuchangia taasisi ya Ali Kimara Rare Didease Foundation, jumla ya shilingi milioni 41 zilipatikana kupitia mapato ya mlangoni na michango iliyotolewa na viongozi wa Serikali, mashirika na watu mbalimbali.

“Tunawashukuru wote ambao wamekuwa pamoja nasi bega kwa bega mpaka kuweza kufika hapa ilikuwa ni furaha na kila mmoja aliweza kuona kile ambacho tulikifanya na tuliweka wazi kwamba yote yatakuwa hadharani,” amesema.

Baada ya dakika 90 ubao wa Uwanja wa Azam Complex ulisoma Yanga 1-1 Somalia ambapo kwa Somalia ni Zakaria alianza kutupia na Chico aliweka usawa kwenye mchezo huo.

SOMA NA HII  BIASHARA UNITED HALI NI TETE,HAKUNA TIKETI ZA KIMATAIFA

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here