Home Habar za Usajili Simba KWA HILI LA MOSES PHIRI….MSIMU UJAO SIMBA MAPEMA TU…YANGA LAZIMA WAMCHUNGE AISEE…

KWA HILI LA MOSES PHIRI….MSIMU UJAO SIMBA MAPEMA TU…YANGA LAZIMA WAMCHUNGE AISEE…


Nyota wa Kimataifa wa Zambia, Moses Phiri amesema atahakikisha anatimiza jukumu lake kubwa la kushinda makombe akiwa na waajiri wake wapya, Simba SC.

Phiri ametangazwa kusajiliwa rasmi na Simba SC jana Juni 15, 2022 baada ya kupita kwa minong’ono ya muda mrefu kuwa nyota huyo atatua Msimbazi ambao juzi hiyo hiyo ndiyo walivuliwa rasmi ubingwa wa Ligi Kuu na watani wao wa jadi, Yanga SC.

Akizungumza mara baada ya kusajiliwa, Phiri amesema anafurahi kujiunga na klabu hiyo kwani ilikuwa ni ndoto yake na kwamba sio kwamba atafunga kila siku lakini kwa uwezo aliokuwa nao atajitahidi kupambana ili awe anashinda.

Phiri amesajiliwa na Simba SC akitokea Klabu ya Zanaco ya nchini Zambia huku akiwa pia ni mchezaji wa timu ya Taifa ya Zambia.

SOMA NA HII  BAADA YA KUIONA YANGA IKITESEKA DHIDI YA SIMBA..SENZO AKUNA KICHWA KISHA AIBUKA NA HILI...

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here