Home Habari za michezo SAA KADHAA KABLA YA SIKU YA WANANCHI…EDO KUMWEMBE AIBUKA NA HILI KUHUSU...

SAA KADHAA KABLA YA SIKU YA WANANCHI…EDO KUMWEMBE AIBUKA NA HILI KUHUSU WASHAMBULIAJI YANGA…AONYA..


Mwandishi wa Habari za Michezo Mwandamizi nchini Tanzania Edo Kumwembe ameonyesha Shauku ya kutaka kuiona safu ya Ushambuliaji ya Mabingwa wa Soka Tanzania Bara Young Africans.

Safu ya Ushambuliaji ya Klabu hiyo Kongwe katika Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, inaundwa na Fiston Mayele, Heritier Makambo, Lazarius Kambole, Stephen Aziz Ki na Bernard Morrison.

Kumwembe ameonesha Shauku hiyo wakati akikichambua kikosi cha Young Africans kupitia Kipindi cha Sports Arena cha Wasafi FM, jana Ijumaa (Agosti 05).

Amesema kuna haja ya kila Mwanachana na Shabiki wa Young Africans kwenda kuitazama timu yake  Jumamosi (Agosti 06), katika mchezo wa Kirafiki dhidi ya Mabingwa wa Uganda Vipers SC, ikiwa ni sehemu ya Shamra Shamra za Siku ya Wananchi, Uwanja wa Benjamin Mkapa.

“Ukiwa shabiki wa Mwananchi na ni katika WIKI YA MWANANCHI ni wakati mzuri kuwatazama Aziz Ki, Fiston Mayele na Bernard Morrison wakicheza pamoja kulisaka lango la wapinzani….usikae home. Hii safu inanipa kahoma flani hivi”

Young Africans itautumia mchezo dhidi ya Vipres SC kama sehemu ya kujiandaa na mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Simba SC, utakaopigwa Jumamosi (Agosti 13), Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam.

SOMA NA HII  BAADA YA MAYELE KUPIGWA BEI ... JINA LA MANZOKI LATAJWA YANGA...'MCHONGO' WOTE HUU HAPA...

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here