Home Habari za michezo KUELEKEA MECHI YA KESHO ….SHIDA KWA ONYANGO BADO IKO PALE PALE…JAMBO LAKE...

KUELEKEA MECHI YA KESHO ….SHIDA KWA ONYANGO BADO IKO PALE PALE…JAMBO LAKE NA SIMBA KUMBE BADO SANA…


Beki kisiki wa Simba SC, Joash Onyango kesho hatakuwa sehemu ya kikos pindi Wekundu hao watakapovaana na KMC kesho Septemba 7, 2022.

Kwa mujibu wa msemaji wa Simba, Ahmed Ally, Onyango hakufanya mazoezi na timu kwa siku kadhaa hivyo hatoweza kucheza na kwamba kuna masuala yake anamalizana na klabu ndipo hatma yake itangazwe.

“Onyango hajafanya mazoezi na wenzake hivyo hatakuwepo kesho katika mchezo wetu dhidi ya KMC. Kuna mambo anayaweka sawa na yatakapokaa sawa tutawaambia lakini ifahamike tu Onyango ni mali yetu na ana mkataba wa miaka miwili,” alisema Ahmed.

SOMA NA HII  TETESI:-TRY AGAIN ASUKA MPANGO WA KUMTOA MO DEWJI SIMBA....BAKHRESA ATAJWA KWENYE MIPANGO...