Home Mechi za Leo Ligi Kuu ULE MPAPATUKO WA MECHI ZA LIGI KUU YA NBC KUENDELEA LEO…HII HAPA...

ULE MPAPATUKO WA MECHI ZA LIGI KUU YA NBC KUENDELEA LEO…HII HAPA RATIBA YA MECHI ZOTE ….


LIGI Kuu Tanzania Bara leo Septemba 6 inaendelea kwa mechi mbili kuchezwa katika viwanja tofauti.

Geita Gold wao watakuwa na kibarua cha kusaka ushindi mbele ya Kagera Sugar, mchezo utakaochezwa Uwanja wa CCM Kirumba.

Geita Gold ipo nafasi ya 13 na pointi moja inakutana na Kagera Sugar iliyo nafasi ya 16 haijakusanya pointi.

Kagera Sugar watakuwa ugenini kusaka pointi tatu ndani ya ligi msimu huu wa 2022/23.

Yanga ipo nafasi ya pili ina pointi sita, Azam FC ipo nafasi ya tano na pointi 4.

Yanga watawakaribisha Azam FC kwenye mchezo unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Mkapa.

Utakuwa ni mchezo wa kwanza Yanga kucheza ikiwa nyumbani huku Azam FC wakicheza mchezo wao wa kwanza ugenini msimu wa 2022/23.

SOMA NA HII  KUHUSU KIPIGO CHA SIMBA JANA...HUU HAPA MTAZAMO WA AMBANGILE KWA UDHAIFU WA AL AHLY...