Home Azam FC A-Z JINSI AZAM FC WALIVYOMALIZANA NA COASTAL UNION NDANI NA NNJE YA...

A-Z JINSI AZAM FC WALIVYOMALIZANA NA COASTAL UNION NDANI NA NNJE YA UWANJA…

MABAO matano yamekusanywa kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara kati ya wenyeji Azam FC na Coastal Union.

Baada ya dakika 90, ubao wa Uwanja wa Azam Complex ulisoma Azam FC 3-2 Coastal Union.

Coastal Union walianza kupata bao la utangulizi dakika ya 14 kupitia kwa Betrand Ngafei lilidumu mpaka muda wa mapumziko.

Kipindi cha pili Azam FC walirejea mchezoni na kufunga kupitia kwa James Akamiko dakika ya 56 kisha dakika 4 mbele Yayha Zayd alipachika bao la pili ilikuwa dakika ya 60 na lile la ushindi lilifungwa na Idd Seleman dakika ya 90.

Kwa upande wa mmiliki wa bao la pili la Coastal Union ni Majimengi aliyepachika bao hilo.

Sasa Azam FC inafikisha pointi 32 ikiwa nafasi ya pili baada ya kucheza mechi 14 za ligi.

SOMA NA HII  JINA LA KIUNGO AZAM FC LAONDOLEWA STARS, MBADALA WAKE HUYU HAPA