Home news KISA KUIKANDIA YANGA …MANZOKI AKIONA CHA MOTO BONGO…MASHABIKI WASHUKA NAYE JUMLA JUMLA..

KISA KUIKANDIA YANGA …MANZOKI AKIONA CHA MOTO BONGO…MASHABIKI WASHUKA NAYE JUMLA JUMLA..

Manzoki ataja siku ya Kujiunga Simba aikataa Yanga hadharani

“Walijua nitavaa nguo za kinyoka nyoka”…. Ni moja ya kauli aliyoitoa mchezaji Ceazar Manzoki alipopewa nafasi ya kuongea kwenye mkutano mkuu wa Simba jana Jumapili.

Kauli hii imepokelewa kwa uchungu mkubwa na Wanajagwani mtandaoni. Manzoki alikua akimaanisha kuwa asingeweza kuchezea timu ya Jangwani kwakua mapenzi yake yake msimbazi.

“Kwa lugha za kejeli alizotoa huyu mwamba ingekuwa ni mchezaji wa Yanga ameongea wapambe wangetoka na mapanga muda huu”

Alianza kulalamika Meneja wa Kitengo cha Digitali wa Yanga, Privadinho kupitia ukurusa wake rasmi wa Twitter. Kama hiyo haitoshi naye mtumiaji wa mtandao huo aitwae “Jkutoe”.

“Ni kweli yaan kuna tatizo kwa waandishi wetu wa habari za michezo hakuna hata mmoja aliyepaza sauti kwa huyu p**ka kutoa Lugha za kashfa Kwa Yanga ila Yanga ndiyo klabu inayowaongezea followers kwenye mitandao ya kijamii.”

Kama hiyo haitoshi nao mashabiki wa Simba wakajitokeza kufanya utani wao kama kawaida.

SOMA NA HII  KUHUSU USAJILI MPYA MSIMBAZI..SENZO EMEFUNGUKA HAYA..!!